Breaking News
recent

YALIYOJIRI KATIKA KIKAO CHA PILI CHA WIZARA YA ELIMU NA WAWAKILISHI WA MADARASA NA IDARA




Kikao Kilifanyika Tarehe 12/04/2019 Katika chumba cha Darasa namba 9. Kikao kilihudhuriwa na Wawakilishi wa Madarasa yaani (CR’s) na Wawakilishi wa Idara mbalimbali yaani (DR’s);
Pia Rais wa Serikali ya Wanafunzi (MISO) Mh. Aziz Juma Hamad na Waziri Mkuu Mh. Athuman Bakene  Walialikwa na kufika katika Kikao hicho.
AJENDA
Ø  Kufungua Kikao
Ø  Utambulisho
Ø  Kusoma Muhtasali wa kikao kilicho pita
Ø  Yatokanayo na kikao kilicho pita
Ø  Uwajibikaji
Ø  Kufunga kikao
Baada ya kikao kufunguliwa na Waziri wa Elimu Mh. Kanal Seif Waziri Mkuu alipewa nafasi ya kuongea machache ambapo alionge kuhusu (01) Viongozi kuwa wazalendo na Serikali yao (02)Uhamasishaji wa watu kufanya mazoezi (03) Nafasi ya kiongozi.
Baada ya hapo Waziri Mkuu Alimkaribisha Rais nae azungumze machache na Rais Alizungumza yafuatayo;  01: Kiongozi kuwa mfano na kioo kwa jamii 02: Kujenga utamaduni wa kujifunza 03: Kujengana ndani ya Ungozi 04: Ahadi zilizo tekelezwa na Serikali ya Wanafunzi (MISO).
CHANGAMOTO
Ø  Wajumbe Kutoka Majimbo tofauti walitoa changamoto zifuatazo nakuonekana ni kikwazo katika suala zima la Taaluma kwa wanafunzi wao;
Ø  Stationery ya MISO kutofunguliwa mapema
Ø  Kusumbua kwa SRMIS na watu kushindwa kuona Course work zao
Ø  Baadhi ya Walimu kuwasumbua watoto wa kike kwa matakwa yao binafsi
Ø  Changamoto ya viti katika Cr4,5,6,7,8 na Cr9
Ø  Baadhi ya Wanafunzi kutopata vitambulisho vyao
Ø  Ukosefu wa taa LT5
Ø  Kuchelewa kwa fedha ya mawasiliano
MWISHO
Waziri wa Elimu Mh. Kanali Seif aliwashukuru wajumbe kuhudhuria katika kikao hicho na kuwa ahidi kuzitafutia ufumbuzi changamoto zote zilizo tajwa na wajumbe, na kuahidi kufanya vikao vingine vya wizara ya Elimu ili kuleta mrejesho wa changamoto zilizo tolewa na wajumbe.
Kikao Kili ahirishwa rasmi saa, 02:08 Usiku



Written By Eston T. Msigala

No comments:

Powered by Blogger.